GREEN ORGANIC PLUS FERTILIZER
Hii ni mbolea isiyo na kemikali hata kidogo, ni mbolea iliyotokana na viumbe hai yani wanyama na mimea. Mbolea ya green world imetengenezwa baada ya utafiti wa kina kufanyika nchini Marekani na kutengenezwa katika viwanda bora zaidi.
Mbolea yetu ya Green world haina madhara kwa binadamu wala wanyama hivyo unaweza kula mazao yako hata baada ya kuitumia, pia imesheheni virutubisho vingi kama vichochezi au homoni,vitamini na madini yote muhimu ambayo huhitajika katika mmea yani macronutrients na micronutrients wakati mbolea nyingi za viwandani huwa na macronutrients tu.Mbolea hii huhifadhiwa katika ujazo wa liter mmoja(1)
VIAMBATA MUHIMU VYA MBOLEA YA GREEN WORLD
Kwakuwa imezingatia mahitaji yote ya mimea ikiwa ni pamoja na virutubisho vyote vinavyohitajika kwa wingi katika mmea (macro nutrients) mbolea hii ina madini ya Nitrogen, Phosphorus, Potassium, Calcium, Magnesium na Sulpher.
Pia mbolea hii ina(micro nutrients) yani madini au virutubishi vyote vinavyohitajika kwa kiwango kidogo katika mmea vikiwa ni Zinc, Ferrous,Copper, Boron,Manganese, Silicon,Molybdenum,Sodium, Cobalt na Chlorine.
Kwakuwa Amino acids ni muhimu katika ukuaji wa mmea, mbolea hii imesheheni aina zote nane za amino acids.Amino acids huusaidia mmea kukua haraka,kuwa na ujazo mkubwa,huusaidia mmea kupambana na magonjwa na nivigumu kuathiriwa na magonjwa mbalimbali.
MAZAO GANI UNAWEZA KUITUMIA MBOLEA YA GREEN WORLD?!
Mbolea ya green world hutumika kunyinyizia mazao au mimea yote haibagui!!!!! hivyo unaweza kuitumia kwa mazao kama nafaka(mahindi,mpunga,ngano,mtama,ulezi n.k),jamii ya mikunde(maharage,kunde,mbaazi,choroko,dengu, n.k) maua,majani ya bustani,miti ya matunda(maembe,mapera,malimau,mapapai n.k) mboga mboga za majani na mazao yenye kutoa matunda(matikitimaji,vitunguu,nyanya,hoho,pilipili,kabeji,spinachi n.k),mazao yanayohifadhi chakula chake ardhini(viazi,vitunguu, karanga,mihogo,njugu mawe,mananasi n.k)mazao ya biashara(pamba,alzeti,karafuu, korosho na kahawa) na mengine mengi.
MATUMIZI YA MBOLEA YA GREEN WORLD
- Mbolea ya green world hutumika kwa kuinyunyizia katika mazao na wakati mwingine kulowekea mbegu.
- Mbolea ya green world huweza kutumika kwa kupandia na kukuzia mazao.
- Kutokana na mbolea hii kusheheni virutubisho vingi zaidi katika ujazo mdogo,unapata fursa ya wewe mtumiaji kuichanganya na maji mengi kabla ya kuitumia ili uweze kuitumia katika eneo kubwa na uwe na matumizi mazuri ya pesa zako.
- Chupa moja(1) ya mbolea utaitumia katika hecta 6.7 au heka 16.5 ninasema hivyo kwa kuwa;
1.Unaweza kuchanganya liter 1 ya mbolea katika liter 1,000/= za maji
2.kama shamba shamba ni dogo yani heka unaweza kuchanganya kifuniko cha mbolea yani mils 50 za mbolea kwa liter 50 za maji nyunyiza mpaka umalize kisha changanya tena kama shamba halijakamilika.
3.kama ni kijibustani unaweza kuchanganya 5mils/5cc za mbolea na ukachanganya na liter 20 za maji.
Angalizo:mbolea hii haiunguzi mazao wala haina madhara kwa mmea hata ikizidishwa vipimo
WAKATI GANI UITUMIE AU UNYUNYIZE MBOLEA YA GREEN WORLD?
Unashauriwa unyinyizie mazao yako katika majani wakati wa alfajiri mpaka asubuhi ambapo jua halijawa kaLi na wakati wa jioni wakati jua limezama,hii ni kwa sababu mmea utafyonza mbolea yote na virutubisho vyote kwani stomata zitakuwa wazi na madini au virutubisho ya mbolea havitaharibiwa kwa jua.
- Unashauriwa uichanganye na maji wakati unataka kuitumia,iwapo itabaki mfano ni àsubuhi basi itumie siku hiyohiyo jioni unyunyizie.
JINSI YA KUNYUNYIZIA MBOLEA HII.
Kuna njia nyingi sana zikiwemo;
- Kubeba kifaa mgongoni chenye dumu na bomba na ukanyunyizia shamba lako.
- Unaweza kumwagilia mbolea katika mazao kwa njia ya drip(drip irrigation)
- katika shamba la miti mirefu unaweza kunyunyiza katika mizizi na matawi
- kutafuta utaratibu wakutengeneza mfumo wa kunyunyiza kama mvua inyeshavyo hasa kama mazao ni mafupi au shamba kubwa sana kama la Maua na mbogamboga.
Haya ni maneeno ya bwana john kutoka songea akirudisha ushuhuda baada ya kutumia mbolea hii ya green organic fertillizer na kupata mafanikio makubwa katika mavuno.
Matokeo/ mabadiliko ya utumiaji wa mbolea
Baada ya kuitumia mbolea hii matokeo mazuri utayaona mapema sana yani baada ya siku saba 7
Faida ya mbolea ya green world
Mbolea hii inakuhakikishia mafanikio yafuatayo;
- kupunguza gharama za kununua mbolea. mfano kikawaida shamba la heka moja hutumia mifuko mitatu ya mbolea ya chumvichumvi, mfuko mmoja wa kilo 50 unaweza kugharimu shilingi 50,000/= mpaka 60,000/=. zidisha kwa mifuko mitatu, 50,000×3=150,000 au 60,000×3=180,000/= sasa hii ni gharama ya kutosha heka 1 pekee. hebu tuangalie gharama ya mbole hiyo hiyo ya chunvuchunvi kwa heka 10. manake ni 150,000×10= 1500,000 (milioni moja na laki 5). HEBU TUANGALIE BEI YA MBOLEA YA GREEN WORLD: chupa moja ya ujazo wa mililita 1000, lita 1 ni sh 90,000, na inatumika kwa heka 8 kama ukipuliza kwa awamu 2. sasa angalia gharama ambayo utakuwa umeepusha. 1500,000-90,000= 1410,000. utakuwa umeokoa zaidi ya shilingi milioni moja kwenye mbolea tu. achilia mbali kuepusha madhara mengine kamakuharibika kwa shamba kutokana na matumizi ya mbolea ya chunvichunvi.
- kuongeza uwezo wa mimea kufyonza madini lishe mbalimbali kutoka katika udongo na pia kuotesha mizizi na matawi haraka.
- kuongeza uwezo wa mimea kujitengenezea chakula chake.
- huongeza rutuba ya shamba lako na inahifadhi unyevu kwa muda mrefu pia hurudisha ph ya udongo kufikia kiwango kinachohitajika kwa mmea yani kati ya 6-8
- huwezesha mimea kuhimili upepo mkali,ukame,baridi na magonjwa
- hufanya mimea kuota mapema na iwe na afya njema n.k
- huongeza thamani ya mazao yako kwani huwa mengi,makubwa,yenye rangi na radha nzuri na yenye kuvutia sana.
Gharama za mbolea kwa chupa 1 ni sh 90,000/= kwa rejareja. na sh 80,000/= kwa chupa kuanzia 3.Ofisi yetu ipo hapa Dar maeneo ya Karume, Machinga Complex . lakini kama upo mkoani usipate shaka tutakutumia mzigo baada ya kufanya malipo.